• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Kondoa District Council
Kondoa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
      • Background
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda ,Biashara na Uwekezaji
      • Planning ,Monitoring and Statistics
      • Huduma za Afya ,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo ,Mifugo na Uvuvi
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Miundombinu, Maendeleo ya Vijiji na Mijini
    • Vitengo
      • Internal Audit
      • Procurement
      • Bee
      • Sheria
      • Information and Communication Technologies (ICT)
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning
      • Mipango na Mazingira
      • Economy ,Health and Education
      • AIDS
      • Maadili
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya Mwenyekiti
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi itakayo Tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

YALIYOJIRI KATIKA SHEREHE ZA MEI MOSI 2017 MKOANI KILIMANJARO

Posted on: May 1st, 2017

Leo ni siku ya wafanyakazi duniani (Mei Mosi). Maadhimisho haya kitaifa yanafanyika mkoa wa Kilimanjaro, Wilaya ya Moshi Mjini katika viwanja vya Ushirika.


Rais Dkt. John Pombe Magufuli ni mgeni rasmi katika sherehe za Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) kitaifa. Shirikisho la Vyama Huru vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) limeandaa sherehe hizi kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU).. Pia wapo viongozi wengine wa kitaifa na mkoa wa Kilimajaro.

Haya ni baadhi ya yaliyojiri wakati wa sherehe za mei mosi na hotuba za viongozi mbalimbali.

Rais TUCTA

- Umma huu unaouona mbele yako unadhihirisha imani kubwa waliyo nayo juu yako.


-Wakati tunaandaa sherehe hizi hatukujua kuwa utakuwa hivi. Umezunguka sehemu mbalimbali lakini hapa umefunika.


Utakapoanza kuongea, utakuwa unaongea na watanzania. Tunaamini TUCTA utatusikiliza.


Miaka yote Serikali haijawahi kuwa hapa mkoa wa Kilimanjaro leo viongozi wote wa serikali wapo mkoa wa Kilimanjaro. Tunaamini yote utakayoongea umma huu wa wafanyakazi utakusikiliza.


Ulituita Ikulu tukakaa na kuzungumzia changamoto na matatizo ya wafanyakazi kwa zaidi ya masaa matatu.


Yapo mengi uliyoahidi kuyazungumzia...

- Ulisema kuhusu kupandishwa madaraja kwa wafanyakazi na tunashukuru umeshashughulikia suala hili.


- Ulituahidi kushughulikia Nyongeza ya mwaka iliyosimama kwa muda mrefu wakati ukirekebisha nchi.


- Ulituahidi kuongeza ajira, Tunashukuru umetangaza ajira zaidi ya 52,000


- Kurejesha jengo letu lililoko Tanga. Tulikwama kwa muda mrefu kulipa deni lakini kwa uwezo wako ndani ya siku tatu tulirejeshewa jengo letu.


Rais wa TUCTA amemaliza na kumkaribisha Rais wa JMT, Dr. Magufuli.


Rais wa JMT, Dr. John Pombe Magufuli

Sijawahi Kuona maadhimisho ya MeiMosi Yaliyofana kama Haya,Mmevunja Record,mmenitia Moyo sana."mapokezi ya leo yamenichanganya kwelikweli ni mapokezi ya aina yake"


Kwakuwa ni mara yangu ya kwanza kufika Kilimanjaro nawashukuru kwa kunipokea na kunipa kura nyingi na kunifanya.


Mei Mosi si kwa ajili ya Tanzania bali duniani kote. Ni siku ya kukumbushana na kutafakari mambo yanayohusu wafanyakazi pamoja na kutatua matatizo yanayowakabili.


Nawapongeza sana wafanyakazi kwa kuadhimisha siku hii muhimu. Pia kuendeleza maendeleo ya Taifa letu. Serikali inawashukuru sana.


Nimesikiliza risala ya katibu Mkuu wa TUCTA. Kama kuna tatizo la kubadilisha sheria za kazi, Spika na Naibu spika wapo hapa.


Nawahakikishia kuwa tunaanza ukurasa mpya. Ndio maana mnaona hii siku ni ya tofauti. Serikali tumeamua kuimarisha maslahi ya wafanyakazi. Na nyie muwe tayari kuchapa kazi.


Wafanyakazi ndio injini ya maendeleo katika taifa lolote kubwa duniani'


Katibu Mkuu wa Tucta kaongea mengi. Mengine ni ya kurekebisha kwa muda mrefe.


Mmeomba kuhusu fao la kazi. Serikali inalifanyia kazi na kuna mchakato unaendelea pindi mfanyakazi anapoacha ajira kabla ya kustaafu basi alipwe sehemu ya mafao.


Kuhusu suala la BIMA, Nawaarifu kuwa serikali inaendelea na utaratibu wa kuanzisha fao la Bima ya ajira na wadau wameshatoa maoni.


Usalama wa kazini (Anaomba aletewe Bango ''Mh. Rais naomba msaada.. Mirathi ya mme wangu sitapata - wasaidizi chukua jina lake).


Uhuru wa wafanyakazi kujiunga na vyama- Hili lishazungumziwa mwaka jana na lipo kwa mujibu wa sheria na hakuna mwajiri aliye juu ya sheria.


Wizara na Taasisi mbalimbali naziagiza kuu kuunda mabaraza ya wafanyakazi. Mpaka sasa kuna mabaraza 478 na bado mabaraza...


Mikataba ya ajira - Hili suala la hiari. Waajiri wote wanatakiwa kutoa mikataba ya ajira makazini. Kinyume chake ni kuvunja sheria.


Kupanda kwa gharama na mfumuko wa bei niwahakikishie kuwa serikali inalishughulikia.


Makato mikopo - Kuna watu wamenufaika na mikopo lakini hawataki kurejesha mikopo hiyo. Hatuwezi kuendelea kuwa tunakopesha na wanapomaliza wanaenda kununua magari na hawataki kurudisha mikopo. Ndio maana tumeweka sheria ili warudishe mikopo haraka.


Serikali inachukua hatua ya kuboresha maslahi ya wafanyakazi.


Serikali ina mapango wa kuboresha na kufufua viwanda. Tukifufua viwanda vijana wetu watapata ajira na TUCTA Itapata wafanyakazi wapya.

Natoa wito kwa wazawa wa kilimanjaro kwa waje wawekeze kwenye mkoa wao kama mzee mengi kwenye Kiwanda cha cocacola.

Hata hivyo kupitia mifuko ya hifadhi ya jamii jumla ya dola za kimarekani milioni 156 zitatumika kujenga viwanda mbalimbali nchini.


Watumishi hewa walikuwa wanatafuna mishahara, wanachukua mikopo. Nilitarajia mwenyekiti wa TUCTA angetoa kauli lakini amepotezea potea kidogo.

Zoezi hili limeenda vizuri na limefikia 98%.


Kuna watumishi wamegushi umri wao wa kustaafu, hawa nao dawa yao tunaichunguza.


Wapo wafanyakazi wenye vyeti feki. Hamna sehemu kwenye sheria za kazi inalazimisha mtu kuajiriwa kwa digrii pekee. Kila mtu anaajiri kuendana na elimu yake.


Katika wafanyakazi 400,035 waliohakikiwa, 9932 wana vyeti feki. Hawa wenye vyeti vya kugushi watupishe.


Nikitaka kupandisha mishahara nitapandisha kwa watumishi kweli, kuna wengine


Nimetoa mpaka kufika tarehe 15 mwezi huu wawe wamejiondoa wenyewe kwenye ajira.

Unapokuwa na watumishi hewa wanakuwa, hawatasita kuandika madai hewa.

Katika kufaniksha kuondoa wafanyakazi hewa na wale wenye vyeti feki.


Kumekuwepo na uhamisho wa walimu ili kupata fedha za uhamisho feki. Sasa niwaombe wafanyakazi, yeyote atakayekuhamisha; Usihame mpaka huyo anayekuhamisha akupe hela za kuhama.


Wengine wanawahamisha kwasababu ya visasi.. Akikuhamisha na cheki yako ya malipo mkononi. Nafikiri wafanyakazi mmenielewa


Tumeamua kununua ndege sita na gharama zetu. Mojawapo ya ndege amabayo inakuja mwaka kesho ina uwezo wa kutoka marekani mpaka KIA. Tunafanya haya kukuza uchumi.


Juzi tumefungua ubalozi wa Israel tumeweza kupata watalii mia nane.


Kwenye bajeti ijayo serikali itaongeza mshahara wa kawaida yaani annual increment.

Nashukuru uongozi wa TUCTA, unapopata viongozi ambao wao ni kutatua matatizo hapo umepata viongozi.


Walimu mlikuwa mnakatwa asilimia mbili ya mshahara ziko wapi?

Mimi sizungumzii, mwaka huu ambayo nitafanya ni haya yaliyoorotheshwa. ni kwenda kutoa promotion kwa wafanyakazi, kupandisha madaraja na tutatoa ajira 52,000.


Sasa ninachowaambia ndugu zangu tuvumiliane,tunazungumzia uchumi wa viwanda uendane na maslahi ya wafanyakazi.

Nawaomba pia tulinde amani na pia tupambane na madawa ya kulevya.

Tutaboresha maslahi ya wafanyakazi.


Sasa ni zamu ya Makamu wa rais, PM na Spika kuwasalimu wana Moshi


Spika: Tutahakikisha sheria zote zinazohusu wafanyakazi zinashughulikiwa kwa haraka.


PM: Wakurugenzi wote wa halmashauri wazingatie agizo la rais la kutowahamisha wafanyakazi bila kuwapa maslahi yao.



Rais Magufuli;

Napenda kuwaambia wana Moshi, Moshi mmevunja rekodi. Ninachowaambia sina cha kuwalipa, nitakachowalipa ni kuwatumikia. Tumepokelewa na Mustahiki Meya, Mbunge na wengine. Na sasa ninajua ya kwamba Moshi mnanipenda.

Najua mlikuwa mnalishwa maneno mengimengi, lakini watanzania wa Moshi na wa maeneo mengine yote wanachohitaji ni maendeleo.


Kwa wafanyakazi wote Tanzania nawaambia; Serikali hii itakuwa mtetezi namba moja ya wafanyakazi.


Tuwe kitu kimoja, kila mmoja akahubiri uzalendo, maendeleo; niwaombe wafanyakazi mkashirikiane na waajiri.

Mimi ningefurahi kwa siku ya Mei mosi tukawape wafanyakazi wote zawadi, najua inawezekana.


Tusibaguane na mimi nina uhakika Mei mosi hii, imekuwa fundisho na natoka hapa ninaenda kukutana na baraza langu la mawaziri kuboresha maslahi ya wafanyakazi.


Mungu awabariki sana.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 06, 2025
  • JEDWALI LA MATUKIO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 24, 2024
  • UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA October 15, 2024
  • Fungua zaidi

Habari Mpya

  • WATUMISHI KONDOA DC WAMPONGEZA MHE.RAIS SAMIA

    May 04, 2025
  • VIONGOZI OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI INAYOFADHILIWA NA FEDHA ZA MFUKO WA JIMBO-KONDOA DC

    May 03, 2025
  • MAJIBU YA HOJA ZA UKAGUZI WA HESABU ZA SERIKALI SASA KUFANYIKA KIDIGITALI

    April 16, 2025
  • MKURUGENZI MILLAO AONGOZA BONANZA LA MNENIA KUELEKEA MWENGE WA UHURU 2025

    April 16, 2025
  • Fungua zaidi

Video

"Kipaumbele changu Kondoa ni Elimu"-Dkt. Ashatu Kijaji(MB)
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Ruhusa
  • Sheria ndogo za Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi portal
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • Chuo cha mipango Dodoma
  • Chuo kikuu Mzumbe
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ajira
  • TAMISEMI
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Wakala ya serikali Mtandao

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo Ramani

Wasiliana Nasi

    KONDOA DISTRICT COUNCIL ,BUKULU VILLAGE

    Anuani ya Posta: Box 1 Kondoa

    Simu : 0262360313

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@kondoadc.go.tz na ded@kondoadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa . Haki zote zimehifadhiwa.